Hivi Mke Wangu Anajiandaa Kuachana na Mimi Baada ya Miaka 10 ya Ndoa au?

Husika na kichwa cha habari, nimekua nikijiuliza hili swali kwa kipindi kirefu sana bila majibu. Mimi na mke wangu tulifunga ndoa ya Kanisani miaka kumi iliyopita, tuna watoto watatu, sisi sote ni wafanyakazi na sote ni masters holders.

Miaka saba iliyopita mke wangu alinifumania na rafiki yake kipenzi. Huyo rafiki alikua anaishi mkoani mara nyingi akija Dar es salaam alikua akifikia kwetu, so akawa amekuja kwa mambo yake.Jumapili moja wife na familia walienda kanisani akabaki rafiki na mimi, baadae nikaenda bar kupata supu, then nikazimua bia kadhaa hadi mchana nikaenda home nilale kidogo nitoke tena.

Nilipofika home nikafungua geti dogo, nilipaki Gari nje. Nikasikia kilio cha mahaba sebuleni naingia hivi namkuta shemeji akiwa na top tu chini hana chochote akijihudumia kwa mkono huku alilia kwa sauti kubwa, nilishindwa kujizuia nikaanza kuvua nguo kama nafukuzwa nikamrukia kochini na akanipokea kwa mikono miwili.

Ikawa ndo mchezo wetu, kumbe housegirl aliunyaka mchezo mzima na kumshtua wife na wakatuwekea mtego ambapo tulinasa, nilikua nimeamka usiku wa nane nikaenda kwa shemeji tukiwa katikati wife akaingia na kutuma na kumtimua rafiki usiku huo huo.Nikamwangukia na kuomba msamaha na nikasamehewa.Miaka michache tangu fumanizi hilo wife akaanzisha tabia ya usiri na kutonishirikisha mambo yake hasa ya maendeleo

(1) Tukio la kwanza:-
Alijenga nyumba sehemu flani hapa Dar es salaam bila mimi kujua, fundi wake alinipa hizo taarifa accidentally
Nilipom confront akakiri na kukosa majibu ya maana.

(2)Tukio la pili:-
Akafungua duka la nguo kimya kimya nikabaini kupitia intelligence info nilizopata akaruka sio duka lake
Ila baadae nilithibitisha ni la kwake.

(3)Tukio la tatu.
Alinunua shamba bagamoyo worth 10 million niligundua baada ya yy kudhulumiwa kumbe Dalali alimtapeli shamba halikua lake.Kesi ikaenda polisi hatimaye mahakamani ikafika pahala ikashindikana kuficha nikagundua, nikaingilia kati kumsaidia mke wangu akarudishiwa pesa zake tukafuta kesi

(4)Tukio la nne
Alinunua Gari 35 million dream car yake, tangu anadunduliza hizo hela akawa anatuma Japan kwa binamu yake kidogo kidogo lakin kimya kimya hadi likafika, nikastukia tu siku amekuja nalo home badala ya kufurahi kwa kweli nilihuzunika

Gari hilo ilibaki kidogo tu liibiwe nikaingilia kati halikuibiwa ilikuaje? Ni hivi:-
Kumbe kijana aliemfanyia clearance bandarini wife hakumlipa yule kijana wakatofautiana
Janki alitaka 1.5 million wife akadai ni laki tano dogo akagomea hela akasema utaona

Baada ya mwezi hilo Gari likaibiwa kibo complex tegeta wife alilia kama mtoto mwanaume nikaingia kazini. Nikatenga kama 1 million kwa polisi, kwa kutumia technolojia ya mawasiliano na kwa ku mtrack yule dogo na mawasiliana yake hatimaye gari ikapatikana dogo yupo nyuma ya nondo hadi leo.

Hata hivyo wife hajaacha hii tabia, hivi sasa ana biashara ya kukopesha watu kwa riba anaifanya kwa siri kubwa ila mimi naijua nimeamua kumuacha tu aendelee maana nimeshachoka.Wadau huyu mtu ana mpango gani na ndoa hii? Au ndo anajiandaa kuishi kivyake baadae? NimefaƱya kosa gani lisilokua na msamaha? Kama lipo naomba mnisaidie majibu ya haya maswali.

Kwa upande wangu, biashara zote nazofanya mbali na kazi yangu anazijua.Hata nyumba nilizojenga nimempeleka kote. Nina guest kijijini kwetu ambayo mama yangu mzazi anaisimamia pia Mke wangu anaijua ingawa ningeweza kumficha na asingejua nipo njia panda najiuliza huyu mtu ni Wa kufa na kuzikana kweli?
Je safari yetu ya maisha ni moja kweli?

Sincerely naomba kwa moyo wenu wa dhati mnisaidie mawazo.

NB: Sijazini tena tangu nizini na Rafiki yake miaka saba iliyopita nae sijawahi kumshika wala kumshuku kwa uzinzi.

HIZI HABARI ZA HIVI ZINAPATIKANA GODSTAR ONLINE >>BONYEZA HAPA KUDOWNLOAD APP YA GODSTAR ONLINE

Comments